Monday, March 25, 2013

TASWIRA NZIMA YA MAHAKAMANI KISUTU LEO.HUKUMU YA KAJALA MASANJA.

Kajala akipandishwa kizimbani kusomewa hukumu.

Kajala na mumewe, Faraja Chambo wakisubiri hukumu yao.…



Kajala akipandishwa kizimbani kusomewa hukumu.

Kajala na mumewe, Faraja Chambo wakisubiri hukumu yao.

Akitafakari.

Akitokwa na machozi baada ya kuhukumiwa. Baba Kajala (kushoto) akishauriana jambo na wasanii wa filamu na maswahiba wa mwanaye.


 
MSANII Kajala Masanja leo ameachiwa huru baada ya kulipiwa faini ya shilingi milioni 13 na Wema Sepetu. Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe, Faraji Agustino kukumbwa na tuhuma za kutakatisha fedha haramu. Katika kesi hiyo, Kajala alihukumiwa kwenda jela miaka 5 au kulipa faini ya shilingi milioni 13. Faraji yeye amehukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 213.


Msaada wa Hari nakujitoa haswaa wa msanii Dr.Cheni pia si wakusahaulika.Ilikua ni kama muendelezo wa alichokifanya kwa Lulu pamoja na Msanii Cloud112 katika mashtaka yao tofauti.Team GaraB inamtakia kila lakheri kwa moyo wake Dr Cheni alkadhalika Wema Sepetu Mungu ndie mpaji sikuzote.
Hongera Kajala.Karibu tena Uraiani.
Picha na GPL.


Monday, March 18, 2013

STORI HII YA TRAFIKI KUGONGWA LEO BAMAGA YATIA SIMANZI SANA..SAMAHANI KWA PICHA HIZI.


Trafiki wa kike aliyejulikana kwa jina moja la Elikiza aliyekuwa akiongoza magari eneo la Bamaga, Mwenge jijini Dar, akifunikwa na wasamaria wema baada ya kugongwa na gari na inadhaniwa kuwa amekufa papo hapo.

Trafiki Elikiza baada ya kugongwa na gari eneo la Bamaga muda huu.

Baadhi ya wananchi waliofika eneo la tukio.

Hali ilivyokuwa eneo la tukio baada ya ajali hiyo.

Trafiki mmoja ambaye amefahamika kwa jina moja la Elikiza, leo amegongwa na gari aina ya VX ambayo haikujulikana namba na inadhaniwa kuwa amekufa papo hapo wakati akiongoza magari eneo la mataa ya Bamaga, Mwenge jijini Dar es Salaam. Taarifa zilizopatikana eneo la tukio zinadai kuwa Trafiki huyo alikuwa akiongoza msafara na baada ya msafara huo, aliruhusu magari mengine yaendelee na safari ndipo ghafla gari lilipotoka upande wa pili na kumgonga.
Chanzo Habari:GPL

Friday, March 15, 2013

HII NDIO VIDEO YA LWAKATARE ILIYOZUA UTATA.SOMA ALICHOSEMA DR.SLAA KUHUSU SAKATA HILO!


Video iliyozua utata hiyo hapo juu.
 
Dk. Slaa pia amelituhumu Jeshi la Polisi kufanya mchezo mchafu kwa maslahi ya kisiasa.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari Makao makuu ya chama hicho kufafanua suala la kushikiliwa kwa Lwakatare.
Dk. Slaa, alilalamikia jeshi la polisi kuwa limekuwa likitumika kisiasa huku akitoa mfano wa chama hicho kuwa kimekuwa kikitaarifu jeshi la polisi kuhusu mambo hayo lakini halijawahi kuchukua hatua.

Alisema  jeshi la polisi halijawahi kuchukua hatua stahiki kwa suala la mauaji ya Daudi Mwangosi kumwajibisha Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Iringa aliyesimamia na kufanikisha kifo cha mwandishi huyo wa habari, jeshi la polisi pia halikuchukua hatua za kumhoji Dk. Stephe Ulimboka baada ya kuteswa na mtu anayedaiwa kuwa ni Afisa wa usalama wa Taifa wa Ikulu, hali kadhalika hawezi kushangaa ikiwa jeshi la polisi halitaacha kumhoji Absalom Kibanda.

Amesema, jeshi la polisi limekuwa likitoa taarifa za kukichafua chama, akikumbushia suala la Mwangosi, alisema kuwa mara tu baada ya tukio la Mwangosi kuuawa, jeshi la Polisi kupitia kwa Kamishna wake lilitoa taarifa kuwa alilipuliwa na kitu kilichorushwa kwake akikimbilia kujisalimisha kwa polisi akitoka kwa wafuasi wa Chadema, jambo ambalo lilikuwa sio kweli.

Hivyo alisema, Mkurugenzi  wa ulinzi na usalama wa Chama hicho kuhusishwa kwa sakata la sasa la mkanda wa video uliopo katika mtandao na Kibanda ni mwendelezo tu wa kukihujumu chama, unaoratibiwa na Usalama wa Taifa, huku ukitekelezwa na jeshi la polisi.

“CHADEMA kinafahamu kwa undani, kwamba uzushi huu wa Tape ya “Bukoba Boy”.Tunajua huu umeanzishwa na kuhusisha Usalama wa Taifa, akiwemo Ighondo na wenziwe pale Ada Estate. Huyu  Ighondo ambaye anafahamika pia kwa jina la “Rama” tunamfahamu vizuri sana," alisema.
 Dk Slaa aliingiza suala la kufungiwa suala la kufungiwa kwa gazeti la MwanaHalisi akiituhumu serikali kutokua makini.

Akakumbushia kuwa waliwahi kutuma barua mbalimbali polisi zinazothibitisha kuwa wanafanyiwa michezo michafu huku zikiwa zimeandikwa majina ya viongozi wa CHADEMA, au taarifa za Vikao vya Chadema zilizopotoshwa lakini polisi hawakuchukua hatua.

Aliongeza kuwa wakati wa uchaguzi wa Igunga walisema kuwa kuna mtu anamiliki bastola isisvyo halali, wakataja hadi namba za bastola iliyoingizwa lakini polisi hawajawahi kushughulika nayo.

Hata hivyo alishangazwa na jeshi la polisi kufanya haraka kumshikilia Lwakatare, kwani vyombo vya habari hivi majuzi vimemtaja kwa majina ya watu kuhusishwa na utekwaji na uteswaji wa Kibanda, lakini jeshi halikusema lolote hadi sasa.

Akaongeza kuwapo watu aliowataja kwa majina kwamba waliingia kwa ID zao kwenye mitandao kukejeli suala la kuteswa Absalom Kibanda lakini jeshi halikuchukua hatua.

Alishangazwa jinsi polisi walivyofanya haraka kumkamata Lwakatare, akasema ni mbinu tu za kukichafua CHADEMA.
 
 

Hadi tunaenda Mitamboni, Jeshi la polisi lilikuwa halijatoa taarifa kuwa Mkurugenzi huyo wa Ulinzi na usalama wa Chadema angepata dhamana au la, lakini Wakili wake alilithibitishia gazeti hili kuwa wameenda tena kumpekua kwa mara nyingine nyumbani kwake.

Kutokana na hali hiyo, Dk Slaa alisisitiza kuwa “madai yaliyotolewa mara nyingi na CHADEMA, kwa Rais kuandikiwa barua na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, iundwe Judicial Commission of Inquiry (Tume Huru ya Kimahakama kuchunguza vifo vyote vyenye utata na sura ya kisiasa).

Akahoji ,Serikali inaogopa nini kuunda Tume hii huru ili ukweli Ujulikane? Iweje CHADEMA inayotuhumiwa Kupanga njama wanaishinikiza Serikali kuunda Chombo huru na Serikali ndiyo inayopata kigugumizi?”

Aliongeza kuwa “kwa wale walioumizwa na kujeruhiwa kama kina Ulimboka Kibanda na wengine, tunarudia Tamko letu la kuwa hatuna Imani na uchunguzi unaofanywa na Jeshi la Polisi kwa kuwa viongozi wa Jeshi hilo ni sehemu ya watu tunaowatuhumu kwa kuhusika kwa njia mbalimbali, na Ushihidi wa wazi na Taarifa mbili za Serikali kupingana yaani Taarifa ya Kamati yqa Nchimbi na Tume ya Haki za Binadamu.

"Tutaiaminije Polisi na Serikali kwa Taarifa ya Kamati ya Nchimbi? Hatuwezi kuendelea kuvumilia ukandamizaji huu wa uhuru wa habari, ambao sasa unaelekea kuota mizizi nchini kwetu. Na kweli ninawaomba na kuwataka waandishi wote msimame imara, bila kujadili itikadi, au tofauti zetu zozote zile na kusimamia uhuru wa Habari. Tunataka vivyo hivyo, kwa wanaharakati mbalimbali. Waache hofu, eti wanaogopa kuhusishwa na vyama vya Siasa! Haki ni haki na haina rangi ya bendera ya chama chochote," alisema.

Azungumzia Bunge:
Dk Slaa amesema kuwa usalama wa Taifa, unafanya kazi kwa maslahi ya Chama cha Mapinduzi hadi ndani ya bunge, ndio maana sasa wabunge wa Chama hicho wameondolewa katika kamati muhimu ambazo walikuwa wanazisimamia, bila wao kuulizwa, tofauti na walivyojaza katika fomu na nje ya ushauri wa Kiongozi wa upinzani bungeni.

Dk slaa alisema hiyo yote ni hujuma, Mnyika amepelekwa Ardhi maliasili na Mazingira, huku Msigwa akiondolewa maliasili na utalii kwa kuwa alikuwa anawataja viongozi wa CCM , jeshi la Polisi, jeshi la Wana nchina Ikulu yenyewe kuhusishwa na ujangili wa wanyama.

Amesikitishwa na wabunge wa Chama chake kuhamishwa kamati muhimu walizokuwa wanazisimamia, huku wengine wakiachwa kuingizwa katika kamati jambo ambalo linawanyima ufuatiliaji wa utendaji wa serikali, ilihali wabunge wengi wa CCM wengine wamewekwa kamati mbili kwa mbunge yule yule.
 
Source:Fikra Pevu.

 

Saturday, February 23, 2013

WHEN IGNAS & STELLA SAYED "YES 4 LIFE" TO EACH OTHER..

 
You can now Call them .Mr & Mrs IGNAS CHONYA .and this 2/2/13was their Day to Remember.

Pingu za Maisha zilivishwa katika Kanisa katoliki la Kristu Mfalme Tbt.

Ignas and  his Lovely Wife Stella,together posing for Camera.

The Reception hosted by the man him self in the  African Print, Mc-GaraB ofcourse. @Highland Hall .It was amaizing..Legooo.

 
Mama Umependeza Sana....




Gara WhaaT!!

I fell in Love with this Cake jamani..Nilikua kama naiona Kashozi vile uo Mji wa mtu unavyoonekana vyema apo..Mpaka zizi la ng'ombe ndani.Lol

1st Image Quality chini yake Mkubwa DAUDI (Dizo Macamera) ndio imekusababisha picha hizo ..Kama umependa kazi yao cheki nao kwa No.0713 222 141.

Thursday, February 21, 2013

RAY APUNGUA UZITO GHAFLA..HOFU YATANDA KWA MASHABIKI WAKE

Msanii Vicent Kigosi /Ray akiwa na Shavu lake sikua chache tu zilizo pita.
Hapa inaonyesha alivyokua Kabla na alivyo sasa.
 
Ray alivyo sasa.
Kila mtu anajiuliza lake tokana na kupungua kwake uzito kwa gafla namna hiyo..Anaumwa,Anamaintain,au ana Stress pengine tokana na ile Movie  yake (Sister Marry) ambayo imezuiliwa na kanisa katoliki..
Wewe kama Mdau unafikiliaje?

THIS IS THE STORY OF MY THURSDAY 21/2 KATIKA PICHA..GARACRAYZ!!

GaraBusy as Usual..
 
 
Somthing Came up ghafla.
 
Ofisini hakukaliki tena..
 
The Phone is F*#%n Busy..
 
Still on Air.
 
Thinking of What to do...Nimevurugwa kwelikweli apa usitake kujua.Niachege tu.
 
Decided to go Out around the street.Fortunately I met with One of ma very long time lovly friend (lost her for 8 years back).When we were both @ O'level..ANGEL.Desent as always, she is a Lawyer right now..Whoow!!She was very suprised and I was suprised too.Atlist she made day,and get out of the stress that i had few minutes ago..The good thing I was the one who recognised her 1st.
 
 
We xchanged the #No as kawa as dawa..Her No Is 0683 7350 wewee acha hizoo ...Hahaha now TunaBonga tu..Good to Meet you again Angel.Keep in Touch.
GaraBig Time.
 
 
 

PADRI EVARIST MUSHI AZIKWA NA MAMIA..HIZI NI PICHA ZA MAZISHI.

 ASkofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Muadham Policup Kadinari Pengo,kwa pamoja na maaskofu wengine wakichomeka Msalaba katika kaburi la marehemu  Padri Evaristus Gabriel Mushi,aliyezikwa jana katika viwanja vya kanisa Katoliki la Kitope, Wilaya ya Kaskazini B Unguja,ambae alifariki Jumapili Iliyopita kwa kupigwa risasi na watu wasiojukanwa.
Rais wa Zanbzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein,(katikati) akiweka shada la mauwa katika kaburi la Marehemu Padri Evaristus Gabriel Mushi,wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jana katika viwanja vya kanisa la Kitope, Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
Continued after the jump ....

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein,(katikati)akifuatana na Askofu wa Kanisa  Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao wakielekea katika Mazishi ya Padri Evaristus Gabriel  Mushi,aliyezikwa katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
 Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga Antony Banzi, akiongoza  sala  wakati wa mazishi ya  Marehemu
 Padri Evaristus Gabriel Mushi,aliyekufa kwa kupigwa risasi Jumapili Iliyopita na kuzikwa leo katika viwanja vya kanisa la Kitope, Wilaya ya kaskazini B Unguja jana.
 Vijana waumini wa Dini ya Kikiristo wakiteremsha jeneza lenye mwili wa marehemu Padri Evaristus Gabriel  Mushi,katika kaburi alilozikwa jana katika viwanja vya kanisa la Katoliki la Kitope, Wilaya ya Kaskazini B Unguja, marehemu alifariki kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita na watu wasiojulikanwa.
 Askofu wa Kanisa  Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao, akitia udongo katika kaburi la Marehemu Padri
Evaristus Gabriel  Mushi,aliyezikwa jana katika viwanja vya kanisa Katoliki la Kitope, Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
 Rais wa Zanbzibar na Mwenyekiti wa Baraza la  mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein, (katikati) akitia udongo  katika kaburi la Marehemu  Padri Evaristus Gabriel  Mushi, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jana katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
 Waziri  wa  Mambo ya Ndani ya Nchi Emanuel Nchimbi ,akitia udongo  katika kaburi la Marehemu  Padri Evaristus Gabriel Mushi, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika jana katika viwanja vya kanisa la Kitope,Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
 Vijana waumini wa Dini ya Kikiristo wakiteremsha udongo wakati wa mazishi ya marehemu  Padri Evaristus Gabriel  Mushi, katika kaburi alilozikwa jana katika viwanja vya kanisa la Katoliki la Kitope, Wilaya ya Kaskazini B Unguja, marehemu alifariki kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita na watu wasiojulikanwa.
 Baadhi ya waumini wa kanisa katoliki  wakiwa katika mazishi ya marehemu  Padri Evaristus Gabriel  Mushi, aliyezikwa jana katika viwanja vya kanisa Katoliki la Kitope, Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
(Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu-Zanzibar)
---
Na Maelezo Zanzibar
Mamia ya Wananchi wa Zanzibar jana wameshiriki Mazishi ya Padri Evaristus Mushi aliyeuwawa kwa kupigwa Risasi na Watu wasiojulikana ambayo yamefanyika katika kijiji cha Kitope Wilaya ya Kaskazini B, Unguja. Katika mazishi hayo Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Shariff Hamad,Viongozi wa Serikali na Vyama vya siasa walihudhuria.
Akitoa salamu za Serikali katika Mazishi hayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Mohammed alisema Serikali imeguswa sana na kifo cha Padri huyo na kuongeza kuwa itahakikisha waliohusika na tukio la mauji hayo wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Anglikacana Michael hafidh amewataka Waamini wa dini ya kikristo kuwa watulivu bila kulipiza kisasi bali waiachie Serikali kufanya kazi yake ili kuwabaini waliopoteza Uhai wa Marehemu huyo.
Awali Mazishi hayo yalitanguliwa na Misa takatifu ya kumuombea Marehemu iliyoendeshwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Dar es Salaam Muadhama Policarp Kadinali Pengo katika Kanisa la Minara Miwili Mjini Zanzibar.
Padri Mushi alifariki dunia Februari 17 baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana wakati akielekea Kanisani kuendesha Misa ya Asubuhi katika Kigangwe cha Mtakatifu Teresia eneo la Beit El Raas mjini Unguja Enzi za uhai wake Padri Mushi alikuwa Msomi wa Shahada ya Uzamivu ya Elimu ya Ushauri nasaha aliyoipata nchini Marekani ambapo umauti ulimkuta akiwa anaelekea kuendesha Ibada ya Jumapili ya kwanza ya Kwarezma.
Padri Evarist Mushi wa Kanisa la Minara Miwili mjini Zanzibar alizaliwa June 15, 1957 Mkoa wa Kilimanjaro akiwa ni mtoto wa nne katika familia ya watoto sita ya Mzee Mushi.
Source:GPL

Wednesday, February 20, 2013

MCHEKI WEMA SEPETU AKIZUNGUMZIA OFISI YAKE MPYA APA..

 


PICHA ZA RAISI WA ZANZIBAR DR SHEIN AKITOA HESHIMA ZA MWISHO KWA FR.EVARIST G MUSHI..

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein (kushoto) akitoa salamu ya Mwisho kwa mwili wa Marehemu Padri Evarest Mushi, katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar, Padri Gabriel Mushi, aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasijuilikana Jumapili iliyopita, na atazikwa leo Kijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja, katikati ni Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia wananchi wakati alipofika katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar kutoa salamu ya Mwisho kwa Padri Evarist Gabriel Mushi, aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasijuilikana Jumapili iliyopita, na atazikwa leo Kijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Augustino Shao wakati alipofika katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar kutoa salamu ya Mwisho kwa Padri Evarist Gabriel Mushi, aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Jumapili iliyopita, na atazikwa leo Kijijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, akitia saini kitabu cha maombolezi ya Padri Evarist Gabriel Mushi, katika Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar, ambapo alifika kutoa salamu ya mwisho kwa Padri huyo, aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasijuilikana Jumapili iliyopita, na atazikwa leo Kijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
 Baadhi ya Waombolezaji wakiwa ndani ya Kanisa la Minaramiwili Mjini Zanzibar wakati wa kutoa salamu ya Mwisho kwa Padri Evarist Gabriel Mushi, aliyefariki kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana Jumapili iliyopita, na atazikwa leo Kijijini Kitope Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
(Picha na Ramadhan Othman Ikulu-Zanzibar)